Kristo yu hai, amefufuka na anaishi kati yetu

“Njooni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu na mjifunze kutoka kwangu, maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu.  Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.” Mathayo 11:28-30

UNGANA NASI

Tunakutana mtandaoni mara tatu kwa wiki. Jumanne, Jumatano na Jumamosi

RATIBA YA SALA

SIKU YA JUMANNE: SAA 3 USIKU MAJIRA YA MASHASHARIKI ( MAREKANI)

SIKU YA JUMATANO: SAA 3 USIKU MAJIRA YA MASHARIKI ( MAREKANI)

SIKU YA JUMAMOSI: SAA 4 ASUBUI MAJIRA YA MASHARIKI ( MAREKANI)

PIGA SIMU KWENDA NAMBA +1-585-1818

MAFUNZO YA BIBLIA

Tusomapo maandiko, Mungu huzungumza nasi na tunabadilishwa. Tunapojifunza Biblia pamoja, Mungu anaahidi kujifunua, kutufundisha jinsi ya kumtii, na kutuonyesha jinsi ya kupendana. Tunapobadilishwa na kuwa kama Yesu, familia zetu, mahali pa kazi na jumuiya zitaathiriwa milele.

MAFUNDISHO YA KANISA

Mafundisho ya kanisa hutoa mfumo mpana wa kuelewa imani, maadili, na jukumu la Kanisa ulimwenguni. Wakatoliki na wasio Wakatoliki wote wanaalikwa kuja kujifunza mafundisho ya Kanisa na kundi la Upya Kiroho, karismatiki katoliki.

“Ninyi, wakarismatiki, mmepokea zawadi kuu kutoka kwa Bwana. Kuzaliwa kwa harakati zenu kulikubaliwa na Roho Mtakatifu kuwa ‘ mkondo wa neema katika Kanisa na kwa Kanisa’. Huu ndio utambulisho wenu: kuwa mkondo wa neema.”

Pope Francis

Jisajili kwa
Kupata Habari zetu